Mwanasiasa lakini pia mwanasheria mashuhuri nchini Kenya amefunguka ya moyoni na kumpasha Diamond Platnumz ya moyoni.
George Wajackoyah mwanasiasa aliyewania kiti cha urais nchini Kenya mwaka jana japokuwa akabwagwa, amemwambia msanii Diamond Platnumz kuwa anafaa kumwomba radhi mzee wake ‘baba yake’ Mzee Abdul ili kumaliza tofauti zilizopo baina yao wawili.

Akizungumza akiwa Arusha wakati alimlaki bwana Silema ameongeza kusema yeye yupo tayari kiwapatanasha wao wawili.
“Mimi niko tayari kuwaita waje tuzungumze ili kumaliza ugomvi wao. Ama tuende New York au Kenya nitawalipia ndege waje tuzungumze” asema Wajackoyah
Aliweka wazi kuwa Yeye binafsi alishawahi kuwa na ugomvi na marehemu baba yake ila ilibidi akamuombe msamaha kabla hajafikwa na umauti wake na akapokea baraka za mzee wake na akapata kumzika vyema alivyoaga.
Je unahisi Wajackoyah ana uwezo wa kupatanisha Diamond Platnumz na mzee wake Juma Abdul?
GIPHY App Key not set. Please check settings