Mambo yanazidi kuchemka kwani viongozi wa Azimio La Umoja hii leo wamekita kambi Nakuru.
Wakiongozwa na kinara wao Baba’ Raila Odinga na Stephen Kalonzo Musyoka, wameongoza mkutano wa kuwarai wakenya kujitokeza tarehe 20,2023 Jumatatu jijini Nairobi ili kushiriki maandamano ya kupinga uongozi wa Rais William Ruto na Naibu wake Gachagua.

Hii inatokana na hali ngumu ya gharama ya maisha inayozidi kupanda kila asubuhi kwani Wakenya wengi wanakufa na Njaa, Wanafunzi hawana karo ya masomo, na kuwa Ruto amekataa Server kufunguliwa ili kudhihirisha matokeo ya uchaguzi wa August 9,2022 ambao Raila anadai ana uhakika wa kutosha kuwa ndiye alishinda uchaguzi huo Kwa kura nyingi zaidi ila IEBC ikauza Uongozi kwake Ruto na team yake.

Hii Leo katika kaunti ya Nakuru, Fatuma ambaye ni Women Representative amepinga vikali uamuzi wa mahakama kuu nchini kenya kuhalalisha Ushoga na Usagaji kwa vijana huku akisema yeye hawezi kukubaliana na maamuzi hayo yanaungwa mkono na serikali ya William Ruto baada ya kupokea msaada wa fesha takariban Bilioni Kumi na Sita (16 Billion) Pesa ya Kenya kutoka Marekani.
“Mimi nimeiva, na ninaingiliwa na Wanaume sio mashoga hao wako statehouse” yeye kasema , Fatuma.
Watch Live Video Hii hapa;
GIPHY App Key not set. Please check settings